| 09.02.2010 | 10:00 UTC
Uchaguzi wa Ukraine, huru na wa haki
KIEV
Mwanasiasa wa upinzani nchini Ukraine, Victor Yanukovich ndiye mshindi dhahiri wa uchaguzi uliokamilika siku ya jumapili. Yanukovich anaongoza kwa asilimia tatu zaidi baada ya aslimia 99 ya kura kuhesabiwa dhidi ya mpinzani wake waziri mkuu Yulia Tymoshenko.
Wasimamizi wa kimataifa wametoa tathmini yao na kuutaja uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki, tangazo ambalo linampa Yanukovich nafasi nzuri zaidi ya kutangazwa rasmi mshindi .
Waziri mkuu Yulia Tymoshenko ana wabunge wengi zaidi katika bunge la Ukraine na huenda kukawa na mvutano zaidi wa uongozi.






